Mipango ya usomaji – Septemba 2020

Mipango ya usomaji – Agosti 2020

Mipango ya usomaji – Julai 2020

Upendo huvumilia, hufadhili

Upendo huvumilia, hufadhili

4  
Upendo huvumilia, hufadhili; upendo hauhusudu; upendo hautakabari; haujivuni

5  
haukosi kuwa na adabu; hautafuti mambo yake; hauoni uchungu; hauhesabu mabaya

6  
haufurahii udhalimu, bali hufurahi pamoja na kweli

7  
huvumilia yote; huamini yote; hutumaini yote; hustahimili yote.

8  
Upendo haupungui neno wakati wo wote; bali ukiwapo unabii utabatilika; zikiwapo lugha, zitakoma; yakiwapo maarifa, yatabatilika.

9  
Kwa maana tunafahamu kwa sehemu; na tunafanya unabii kwa sehemu

10  
lakini ijapo ile iliyo kamili, iliyo kwa sehemu itabatilika.

11  
Nilipokuwa mtoto mchanga, nalisema kama mtoto mchanga, nalifahamu kama mtoto mchanga, nalifikiri kama mtoto mchanga; tokea hapo nilipokuwa mtu mzima, nimeyabatilisha mambo ya kitoto.

12  
Maana wakati wa sasa tunaona kwa kioo kwa jinsi ya fumbo; wakati ule tutaona uso kwa uso; wakati wa sasa nafahamu kwa sehemu; wakati ule nitajua sana kama mimi nami ninavyojuliwa sana.

13  
Basi, sasa inadumu imani, tumaini, upendo, haya matatu; na katika hayo lililo kuu ni upendo.

1 Corinthians 13 in Swahili

1 Corinthians 13 in English