|
Zab 23: BWANA ndiye mchungaji wangu

1
BWANA ndiye mchungaji wangu, Sitapungukiwa na kitu.
2
Katika malisho ya majani mabichi hunilaza, Kando ya maji ya utulivu huniongoza.
3
Hunihuisha nafsi yangu; na kuniongoza Katika njia za haki kwa ajili ya jina lake.
4
Naam, nijapopita kati ya bonde la uvuli wa mauti, Sitaogopa mabaya; Kwa maana Wewe upo pamoja nami, Gongo lako na fimbo yako vyanifariji.
5
Waandaa meza mbele yangu, Machoni pa watesi wangu. Umenipaka mafuta kichwani pangu, Na kikombe changu kinafurika.
6
Hakika wema na fadhili zitanifuata Siku zote za maisha yangu; Nami nitakaa nyumbani mwa BWANA milele.
BibleProject: Mihtasari ya Vitabu: Agano Jipya: Warumi
Tafakari umbo na mada msingi za kila kitabu cha Biblia kupitia maelezo ya mfano.
|
Mtu ye yote akitaka kunifuata, na ajikane mwenyewe, ajitwike msalaba wake, anifuate
BibleProject: Mihtasari ya Vitabu: Agano Jipya: Luka – Matendo
Tafakari umbo na mada msingi za kila kitabu cha Biblia kupitia maelezo ya mfano.
|
|
|
|
|