Gundua programu nyepesi ya Biblia ya nje ya mtandao kutoka kwa YouVersion!

Programu mpya ya Biblia iko hapa!

Inapatikana kwa Android
barani Afrika na Asia


YouVersion Biblia Takatifu Lite

Tayari kwenye zaidi ya vifaa milioni 2.7, programu hii mpya inakupa ufikiaji kamili wa nje ya mtandao kwa vipengele muhimu vya Bible App—yote huku ukifanya nafasi ya kuhifadhi simu yako kuwa nyepesi.

Soma Biblia nje ya mtandao, pata Sala za Kila Siku, shiriki mistari ya Biblia, sikiliza sauti za Biblia, na mengine mengi.

Endelea kushikamana na Mungu kupitia Neno Lake wakati wowote, mahali popote!

Iwapo unatafuta programu ya Biblia ya kila mtu-moja iliyo nje ya mtandao, matoleo tofauti na sauti—usitafute kwingine.
~ Davor, Nigeria

Pata Programu Bila Malipo


Helpful links:
YouVersion Biblia Takatifu Lite (na África)
Apu ya Biblia ya Watoto

Biblia i Hai

Biblia i Hai

Maana Neno la Mungu li hai, tena lina nguvu, tena lina ukali kuliko upanga uwao wote ukatao kuwili, tena lachoma hata kuzigawanya nafsi na roho, na viungo na mafuta yaliyomo ndani yake; tena li jepesi kuyatambua mawazo na makusudi ya moyo.

Ebr 4:12

Biblia i Hai

Zab 23: BWANA ndiye mchungaji wangu

1  
BWANA ndiye mchungaji wangu, Sitapungukiwa na kitu.

2  
Katika malisho ya majani mabichi hunilaza, Kando ya maji ya utulivu huniongoza.

3  
Hunihuisha nafsi yangu; na kuniongoza Katika njia za haki kwa ajili ya jina lake.

4  
Naam, nijapopita kati ya bonde la uvuli wa mauti, Sitaogopa mabaya; Kwa maana Wewe upo pamoja nami, Gongo lako na fimbo yako vyanifariji.

5  
Waandaa meza mbele yangu, Machoni pa watesi wangu. Umenipaka mafuta kichwani pangu, Na kikombe changu kinafurika.

6  
Hakika wema na fadhili zitanifuata Siku zote za maisha yangu; Nami nitakaa nyumbani mwa BWANA milele.

Psalm 23 in Swahili

Psalm 23 in English – NKJV

BibleProject: Mihtasari ya Vitabu: Agano Jipya: Warumi

BibleProject: Mihtasari ya Vitabu - Agano Jipya

Tafakari umbo na mada msingi za kila kitabu cha Biblia kupitia maelezo ya mfano.

Muhtasari: Warumi 1-4

Muhtasari: Warumi 5-16

Mtu ye yote akitaka kunifuata, na ajikane mwenyewe, ajitwike msalaba wake, anifuate

Mtu ye yote akitaka kunifuata, na ajikane mwenyewe, ajitwike msalaba wake, anifuate

Yesu akamkazia macho, akampenda, akamwambia, Umepungukiwa na neno moja. Enenda, ukauze ulivyo navyo vyote, uwape maskini, nawe utakuwa na hazina mbinguni; kisha njoo unifuate. Walakini yeye akakunja uso kwa neno hilo, akaenda zake kwa huzuni; kwa sababu alikuwa na mali nyingi.

Mk 10:21-22

Akawaita mkutano pamoja na wanafunzi wake, akawaambia, Mtu ye yote akitaka kunifuata na ajikane mwenyewe, ajitwike na msalaba wake, anifuate. Kwa kuwa mtu atakaye kuiponya nafsi yake, ataiangamiza, na mtu atakayeiangamiza nafsi yake kwa ajili yangu na kwa ajili ya Injili, huyu ataisalimisha.

Mk 8:34-35

Wala mtu asiyechukua msalaba wake akanifuata, hanistahili.

Mt 10:38

Nimesulibiwa pamoja na Kristo; lakini ni hai; wala si mimi tena, bali Kristo yu hai ndani yangu; na uhai nilio nao sasa katika mwili, ninao katika imani ya Mwana wa Mungu, ambaye alinipenda, akajitoa nafsi yake kwa ajili yangu.

Gal 2:20

Akawaambia wote, Mtu ye yote akitaka kunifuata, na ajikane mwenyewe, ajitwike msalaba wake kila siku, anifuate. Kwa kuwa mtu atakaye kuiponya nafsi yake ataiangamiza, na mtu atakayeiangamiza nafsi yake kwa ajili yangu ndiye atakayeisalimisha. Kwa kuwa yamfaa nini mtu kuupata ulimwengu wote, kama akijiangamiza, au kujipoteza mwenyewe?

Lk 9:23-25

akisema, Ee Baba, ikiwa ni mapenzi yako, uniondolee kikombe hiki; walakini si mapenzi yangu, bali yako yatendeke. [ Malaika kutoka mbinguni akamtokea akamtia nguvu.

Lk 22:42-43

Na hao walio wa Kristo Yesu wameusulibisha mwili pamoja na mawazo yake mabaya na tamaa zake.

Gal 5:24

Wakati huo Yesu aliwaambia wanafunzi wake, Mtu ye yote akitaka kunifuata, na ajikane mwenyewe, ajitwike msalaba wake, anifuate. Kwa kuwa mtu atakaye kuiokoa nafsi yake, ataipoteza; na mtu atakayepoteza nafsi yake kwa ajili yangu, ataiona. Kwani atafaidiwa nini mtu akiupata ulimwengu wote, na kupata hasara ya nafsi yake? Au mtu atatoa nini badala ya nafsi yake? Kwa sababu Mwana wa Adamu atakuja katika utukufu wa Baba yake pamoja na malaika zake; ndipo atakapomlipa kila mtu kwa kadiri ya matendo yake.

Mt 16:24-27

Kwa maana nayahesabu mateso ya wakati huu wa sasa kuwa si kitu kama utukufu ule utakaofunuliwa kwetu.

Rum 8:18

Heri mtu astahimiliye majaribu; kwa sababu akiisha kukubaliwa ataipokea taji ya uzima, Bwana aliyowaahidia wampendao.

Yak 1:12