BibleProject: Mihtasari ya Vitabu: Agano Jipya: Luka – Matendo

BibleProject: Mihtasari ya Vitabu - Agano Jipya

Tafakari umbo na mada msingi za kila kitabu cha Biblia kupitia maelezo ya mfano.

Muhtasari: Luka 1-9

Muhtasari: Luka 10-24

Muhtasari: Matendo 1-12

Mipango ya usomaji – Juni 2021

Zaburi 91 – Bwana ndiye kimbilio langu na ngome yangu

1  
Aketiye mahali pa siri pake Aliye juu Atakaa katika uvuli wake Mwenyezi.

2  
Nitasema, BWANA ndiye kimbilio langu na ngome yangu, Mungu wangu nitakayemtumaini.

3  
Maana Yeye atakuokoa na mtego wa mwindaji, Na katika tauni iharibuyo.

4  
Kwa manyoya yake atakufunika, Chini ya mbawa zake utapata kimbilio; Uaminifu wake ni ngao na kigao.

5  
Hutaogopa hofu ya usiku, Wala mshale urukao mchana

6  
Wala tauni ipitayo gizani, Wala uele uharibuo adhuhuri

7  
Ijapo watu elfu waanguka ubavuni pako. Naam, kumi elfu mkono wako wa kuume! Hata hivyo hautakukaribia wewe.

8  
Ila kwa macho yako utatazama, Na kuyaona malipo ya wasio haki.

9  
Kwa kuwa Wewe BWANA ndiwe kimbilio langu; Umemfanya Aliye juu kuwa makao yako.

10  
Mabaya hayatakupata wewe, Wala tauni haitaikaribia hema yako.

11  
Kwa kuwa atakuagizia malaika zake Wakulinde katika njia zako zote.

12  
Mikononi mwao watakuchukua, Usije ukajikwaa mguu wako katika jiwe.

13  
Utawakanyaga simba na nyoka, Mwana-simba na joka utawaseta kwa miguu.

14  
Kwa kuwa amekaza kunipenda Nitamwokoa; na kumweka palipo juu, Kwa kuwa amenijua Jina langu.

15  
Ataniita nami nitamwitikia; Nitakuwa pamoja naye taabuni, Nitamwokoa na kumtukuza

16  
Kwa siku nyingi nitamshibisha, Nami nitamwonyesha wokovu wangu.

BibleProject: Mihtasari ya Vitabu: Agano Jipya: Mathayo – Yohana

BibleProject: Mihtasari ya Vitabu - Agano Jipya

Tafakari umbo na mada msingi za kila kitabu cha Biblia kupitia maelezo ya mfano.

Muhtasari: Mathayo 1-13

Muhtasari: Mathayo 14-28

Muhtasari: Marko

Muhtasari: Yohana 1-12

Muhtasari: Yohana 13-21

Mimi ndimi nuru ya ulimwengu

Mimi ndimi nuru ya ulimwengu

Basi Yesu akawaambia tena akasema, Mimi ndimi nuru ya ulimwengu, yeye anifuataye hatakwenda gizani kamwe, bali atakuwa na nuru ya uzima.


Yn 8:12

Watu wale waliokwenda katika giza Wameona nuru kuu; Wale waliokaa katika nchi ya uvuli wa mauti, Nuru imewaangaza.


Isa 9:2

BWANA ni nuru yangu na wokovu wangu, Nimwogope nani? BWANA ni ngome ya uzima wangu, Nimhofu nani?


Zab 27:1

Kwa kuwa Mungu, aliyesema, Nuru itang’aa toka gizani, ndiye aliyeng’aa mioyoni mwetu, atupe nuru ya elimu ya utukufu wa Mungu katika uso wa Yesu Kristo.


2 Kor 4:6

Na Kristo akiwa ndani yenu, mwili wenu umekufa kwa sababu ya dhambi; bali roho yenu i hai, kwa sababu ya haki. Lakini, ikiwa Roho yake yeye aliyemfufua Yesu katika wafu anakaa ndani yenu, yeye aliyemfufua Kristo Yesu katika wafu ataihuisha na miili yenu iliyo katika hali ya kufa, kwa Roho wake anayekaa ndani yenu.


Rum 8:10-11

Kwa maana zamani ninyi mlikuwa giza, bali sasa mmekuwa nuru katika Bwana; enendeni kama watoto wa nuru


Efe 5:8

bali tukienenda nuruni, kama yeye alivyo katika nuru, twashirikiana sisi kwa sisi, na damu yake Yesu, Mwana wake, yatusafisha dhambi yote. Tukisema kwamba hatuna dhambi, twajidanganya wenyewe, wala kweli haimo mwetu. Tukiziungama dhambi zetu, Yeye ni mwaminifu na wa haki hata atuondolee dhambi zetu, na kutusafisha na udhalimu wote.


1 Yoh 1:7-9

Ninyi ni nuru ya ulimwengu. Mji hauwezi kusitirika ukiwa juu ya mlima. Wala watu hawawashi taa na kuiweka chini ya pishi, bali juu ya kiango; nayo yawaangaza wote waliomo nyumbani. Vivyo hivyo nuru yenu na iangaze mbele ya watu, wapate kuyaona matendo yenu mema, wamtukuze Baba yenu aliye mbinguni.


Mt 5:14-16

Nayo nuru yang’aa gizani, wala giza halikuiweza.


Yn 1:5