Mipango ya usomaji – Julai 2019

Hesabuni ya kuwa ni furaha tupu, mkiangukia katika majaribu mbalimbali

Hesabuni ya kuwa ni furaha tupu, mkiangukia katika majaribu mbalimbali

2  
Ndugu zangu, hesabuni ya kuwa ni furaha tupu, mkiangukia katika majaribu mbalimbali

3  
mkifahamu ya kuwa kujaribiwa kwa imani yenu huleta saburi.

4  
Saburi na iwe na kazi kamilifu, mpate kuwa wakamilifu na watimilifu bila kupungukiwa na neno.

5  
Lakini mtu wa kwenu akipungukiwa na hekima, na aombe dua kwa Mungu, awapaye wote, kwa ukarimu, wala hakemei; naye atapewa.

6  
Ila na aombe kwa imani, pasipo shaka yo yote; maana mwenye shaka ni kama wimbi la bahari lililochukuliwa na upepo, na kupeperushwa huku na huku.

7  
Maana mtu kama yule asidhani ya kuwa atapokea kitu kwa Bwana.

8  
Mtu wa nia mbili husita-sita katika njia zake zote.

9  
Lakini ndugu asiye na cheo na afurahi kwa kuwa ametukuzwa

10  
bali tajiri kwa kuwa ameshushwa; kwa maana kama ua la majani atatoweka.

11  
Maana jua huchomoza kwa hari, huyakausha majani; ua lake huanguka, uzuri wa umbo lake hupotea; vivyo hivyo naye tajiri atanyauka katika njia zake.

12  
Heri mtu astahimiliye majaribu; kwa sababu akiisha kukubaliwa ataipokea taji ya uzima, Bwana aliyowaahidia wampendao.

James 1 in Swahili

James 1 in English

Mipango ya usomaji – Juni 2019

Umkabidhi Bwana njia yako, Pia umtumaini, naye atafanya

Umkabidhi Bwana njia yako, Pia umtumaini, naye atafanya

1  
Usikasirike kwa sababu ya watenda mabaya, Usiwahusudu wafanyao ubatili.

2  
Maana kama majani watakatika mara, Kama miche mibichi watanyauka.

3  
Umtumaini BWANA ukatende mema, Ukae katika nchi, upendezwe na uaminifu.

4  
Nawe utajifurahisha kwa BWANA, Naye atakupa haja za moyo wako.

5  
Umkabidhi BWANA njia yako, Pia umtumaini, naye atafanya.

6  
Ataitokeza haki yako kama nuru, Na hukumu yako kama adhuhuri.

7  
Ukae kimya mbele za BWANA, Nawe umngojee kwa saburi; Usimkasirikie yeye afanikiwaye katika njia yake, Wala mtu afanyaye hila.

8  
Ukomeshe hasira, uache ghadhabu, Usikasirike, mwisho wake ni kutenda mabaya.

9  
Maana watenda mabaya wataharibiwa, Bali wamngojao BWANA ndio watakaoirithi nchi.

10  
Maana bado kitambo kidogo asiye haki hatakuwapo, Utapaangalia mahali pake wala hatakuwapo.

11  
Bali wenye upole watairithi nchi, Watajifurahisha kwa wingi wa amani.

Psalm 37 in Swahili

Psalm 37 in English

Mke mwema, ni nani awezaye kumwona?

Mke mwema, ni nani awezaye kumwona?

10  
Mke mwema, ni nani awezaye kumwona? Maana kima chake chapita kima cha marijani.

11  
Moyo wa mumewe humwamini, Wala hatakosa kupata mapato.

12  
Humtendea mema wala si mabaya, Siku zote za maisha yake.

13  
Hutafuta sufu na kitani; Hufanya kazi yake ya mikono kwa moyo.

14  
Afanana na merikebu za biashara; Huleta chakula chake kutoka mbali.

15  
Tena huamka, kabla haujaisha usiku; Huwapa watu wa nyumbani mwake chakula; Na wajakazi wake sehemu zao.

16  
Huangalia shamba, akalinunua; Kwa mapato ya mikono yake hupanda mizabibu.

17  
Hujifunga nguvu viunoni kama mshipi; Hutia mikono yake nguvu.

18  
Huona kama bidhaa yake ina faida; Taa yake haizimiki usiku.

19  
Hutia mikono yake katika kusokota; Na mikono yake huishika pia.

20  
Huwakunjulia maskini mikono yake; Naam, huwanyoshea wahitaji mikono yake.

21  
Hawahofii theluji watu wa nyumbani mwake; Maana wote wa nyumbani mwake huvikwa nguo nyekundu.

22  
Hujifanyia mazulia ya urembo; Mavazi yake ni kitani safi na urujuani.

23  
Mume wake hujulikana malangoni; Aketipo pamoja na wazee wa nchi.

24  
Hufanya nguo za kitani na kuziuza; Huwapa wafanya biashara mishipi.

25  
Nguvu na hadhi ndiyo mavazi yake; Anaucheka wakati ujao.

26  
Hufumbua kinywa chake kwa hekima, Na sheria ya wema i katika ulimi wake.

27  
Huangalia sana njia za watu wa nyumbani mwake; Wala hali chakula cha uvivu.

28  
Wanawe huondoka na kumwita heri; Mumewe naye humsifu, na kusema

29  
Binti za watu wengi wamefanya mema, Lakini wewe umewapita wote.

30  
Upendeleo hudanganya, na uzuri ni ubatili; Bali mwanamke amchaye BWANA, ndiye atakayesifiwa.

31  
Mpe mapato ya mikono yake, Na matendo yake yamsifu malangoni.

Proverbs 31 in Swahili

Proverbs 31 in English