Mistari maarufu ya Biblia – Machi 2021 – Ikiwa watu wangu…

Maana Mungu hakutupa roho ya woga, bali ya nguvu na ya upendo na ya moyo wa kiasi.


2 Tim 1:7

Nikizifunga mbingu isiwe mvua, tena nikiamuru nzige kula nchi, au nikiwapelekea watu wangu tauni; ikiwa watu wangu, walioitwa kwa jina langu, watajinyenyekesha, na kuomba, na kunitafuta uso, na kuziacha njia zao mbaya; basi, nitasikia toka mbinguni, na kuwasamehe dhambi yao, na kuiponya nchi yao.


2 Nya 7:13-14

usiogope, kwa maana mimi ni pamoja nawe; usifadhaike, kwa maana mimi ni Mungu wako; nitakutia nguvu, naam, nitakusaidia, naam, nitakushika kwa mkono wa kuume wa haki yangu.


Isa 41:10

Njoni, watu wangu, ingia wewe ndani ya vyumba vyako, ukafunge mlango nyuma yako ujifiche kitambo kidogo, mpaka ghadhabu hii itakapopita. Kwa maana, tazama, BWANA anakuja kutoka mahali pake, ili kuwaadhibu wakaao duniani, kwa sababu ya uovu wao; ardhi nayo itafunua damu yake, wala haitawafunika tena watu wake waliouawa.


Isa 26:20-21

Najikumbusha neno hili,Kwa hiyo nina matumaini.Ni huruma za BWANA kwamba hatuangamii,Kwa kuwa rehema zake hazikomi.Ni mpya kila siku asubuhi;Uaminifu wako ni mkuu.BWANA ndiye fungu langu, husema nafsi yangu,Kwa hiyo nitamtumaini yeye.


Omb 3:21-24

Heri mtu astahimiliye majaribu; kwa sababu akiisha kukubaliwa ataipokea taji ya uzima, Bwana aliyowaahidia wampendao.


Yak 1:12

Lakini msisahau kutenda mema na kushirikiana; maana sadaka kama hizi ndizo zimpendezazo Mungu.


Ebr 13:16

Aketiye mahali pa siri pake Aliye juuAtakaa katika uvuli wake Mwenyezi.Nitasema, BWANA ndiye kimbilio langu na ngome yangu,Mungu wangu nitakayemtumaini.


Zab 91:1-2