Mipango ya usomaji – Mei 2019

App ya Biblia ya Watoto sasa inalinganisha vyombo vyote!

Maelezo kayika App ya Biblia ya Watoto

“Hey! Nyota zangu zote ziko!”

Mbele, tuzo za watoto wako zimehifadhiwa kwenye chombo ambapo walizopata. Ikiwa walipata chombo mpya, ao ikiwa uliwaruhusia kutumia App ya Biblia ya Watoto kwenye simu ingine, walipaswa kuanza upya mwanzo. Sivyo tena.

Sasa maendeleo imehifadhiwa kwa kila mmoja wa watoto wako, imeunganishwa kwenye vyombo vyako vyote!

Kama mzazi au mlezi, usasisha wa sasa wa App ya Biblia ya Watoto inakuwezesha kuingia kwa kutumia daftari ya YouVersion ilipo yako na kuanzisha avatari kipekee kwa kila mtoto. Kuongeza maelezo ni haraka na rahisi. Watoto wako wanaweza hata kuchagua avatari na rangi zao.

Pata App ilisasaishwa

Ombeni, nanyi mtapewa; tafuteni, nanyi mtaona; bisheni, nanyi mtafunguliwa;

Ombeni, nanyi mtapewa; tafuteni, nanyi mtaona; bisheni, nanyi mtafunguliwa;

7  
Ombeni, nanyi mtapewa; tafuteni, nanyi mtaona; bisheni, nanyi mtafunguliwa

8  
kwa maana kila aombaye hupokea; naye atafutaye huona; naye abishaye atafunguliwa.

9  
Au kuna mtu yupi kwenu, ambaye, mwanawe akimwomba mkate, atampa jiwe?

10  
Au akiomba samaki, atampa nyoka?

11  
Basi ikiwa ninyi, mlio waovu, mnajua kuwapa watoto wenu vipawa vyema, je! Si zaidi sana Baba yenu aliye mbinguni atawapa mema wao wamwombao?

12  
Basi yo yote myatakayo mtendewe na watu, nanyi watendeeni vivyo hivyo; maana hiyo ndiyo torati na manabii.

Matthew 7 in Swahili

Matthew 7 in English

Heri walio maskini wa roho

Heri walio maskini wa roho

3  
Heri walio maskini wa roho; Maana ufalme wa mbinguni ni wao.

4  
Heri wenye huzuni; Maana hao watafarijika.

5  
Heri wenye upole; Maana hao watairithi nchi.

6  
Heri wenye njaa na kiu ya haki; Maana hao watashibishwa.

7  
Heri wenye rehema; Maana hao watapata rehema.

8  
Heri wenye moyo safi; Maana hao watamwona Mungu.

9  
Heri wapatanishi; Maana hao wataitwa wana wa Mungu.

10  
Heri wenye kuudhiwa kwa ajili ya haki; Maana ufalme wa mbinguni ni wao.

11  
Heri ninyi watakapowashutumu na kuwaudhi na kuwanenea kila neno baya kwa uongo, kwa ajili yangu.

12  
Furahini, na kushangilia; kwa kuwa thawabu yenu ni kubwa mbinguni; kwa maana ndivyo walivyowaudhi manabii waliokuwa kabla yenu.

Matthew 5 in Swahili

Matthew 5 in English

Heri mtu yule asiyekwenda Katika shauri la wasio haki

Heri mtu yule asiyekwenda Katika shauri la wasio haki

1  
Heri mtu yule asiyekwenda Katika shauri la wasio haki; Wala hakusimama katika njia ya wakosaji; Wala hakuketi barazani pa wenye mizaha.

2  
Bali sheria ya BWANA ndiyo impendezayo, Na sheria yake huitafakari mchana na usiku.

3  
Naye atakuwa kama mti uliopandwa Kandokando ya vijito vya maji, Uzaao matunda yake kwa majira yake, Wala jani lake halinyauki; Na kila alitendalo litafanikiwa.

4  
Sivyo walivyo wasio haki; Hao ni kama makapi yapeperushwayo na upepo.

5  
Kwa hiyo wasio haki hawatasimama hukumuni, Wala wakosaji katika kusanyiko la wenye haki.

6  
Kwa kuwa BWANA anaijua njia ya wenye haki, Bali njia ya wasio haki itapotea.

Psalm 1 in Swahili

Psalm 1 in English