Heri walio maskini wa roho

Heri walio maskini wa roho

3  
Heri walio maskini wa roho; Maana ufalme wa mbinguni ni wao.

4  
Heri wenye huzuni; Maana hao watafarijika.

5  
Heri wenye upole; Maana hao watairithi nchi.

6  
Heri wenye njaa na kiu ya haki; Maana hao watashibishwa.

7  
Heri wenye rehema; Maana hao watapata rehema.

8  
Heri wenye moyo safi; Maana hao watamwona Mungu.

9  
Heri wapatanishi; Maana hao wataitwa wana wa Mungu.

10  
Heri wenye kuudhiwa kwa ajili ya haki; Maana ufalme wa mbinguni ni wao.

11  
Heri ninyi watakapowashutumu na kuwaudhi na kuwanenea kila neno baya kwa uongo, kwa ajili yangu.

12  
Furahini, na kushangilia; kwa kuwa thawabu yenu ni kubwa mbinguni; kwa maana ndivyo walivyowaudhi manabii waliokuwa kabla yenu.

Matthew 5 in Swahili

Matthew 5 in English